Home Makala Mwashinga Agonganisha Vilabu Ligi Kuu

Mwashinga Agonganisha Vilabu Ligi Kuu

kiungo huyo James Mwashinga kutoka katika klabu ya Pamba Jiji Fc

by Dennis Msotwa
0 comments
Mwashinga - sportsleo.co.tz

Klabu ya JKT Tanzania ipo katika hatua nzuri ya kukamilisha usajili wa kiungo James Mwashinga kutoka katika klabu ya Pamba Jiji Fc ambae mkataba wake umeisha klabuni hapo.

Mpaka sasa kuna vita Kubwa sana ya kumnasa kiungo huyo fundi ambae alikuwa na msimu bora sana na wanalindanda akicheza maeneo muhimu ya ulinzi na kiungo.

Mbali na Jkt Tanzania pia klabu za KMC na Tabora United zote zinahitaji huduma ya Mwashinga huku JKT Tanzania ikipenya moja Kwa moja mstari wa mbela kutokana na ofa walizoweka mezani Kwa Mwashinga.

banner

Pia bado Pamba Jiji Fc inamuhitaji kiungo huyo kusalia klabuni hapo ambapo amekua na faida kubwa kiufundi akicheza kama mshambuliaji wa pili sambamba na nafasi zote za kiungo pamoja na beki wa kati.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited