Home Soka Mzamiru Yupo Sana Simba Sc

Mzamiru Yupo Sana Simba Sc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba Sc imetangaza kumbakisha Mzamiru ndani ya viunga vya Msimbazi kwa miaka miwili ijayo baada ya kukubali kumuongezea mkataba wa miaka miwili utakaodumu mpaka Juni 31 2026.

Mzimiru ameibuka kuwa moja ya wachezaji tegemeo klabuni hapo tangu alipojiunga na klabu hiyo mwaka 2016 akitokea Mtibwa Sugar ambapo licha ya changamoto za kuletewa mastaa wa kigeni eneo la kiungo Mzimiru hajawahi kuteteleka.

banner

Mkataba wa awali wa kiungo huyo unafikia tamati juni 31 mwaka huu na sasa pamoja na marekebisho makubwa ya kikosi kiungo huyo anaendelea kusalia klabuni hapo ambapo analetewa mastaa wa maana kuja kushindania nafasi.

Eneo la kiungo la Simba sc msimu uliopita lilitawaliwa na Fabrice Ngoma ambaye alikua panga pangua huku Mzamiru Yassin,Sadio Kanoute,Abdalah Hamis wakipishana mara kwa mara eneo hilo.

Mpaka sasa sambamba na mazungumzo kuendelea baina ya klabu hiyo na wachezaji kadhaa wa ndani na nje ya nchi ili wajiunge na klabu hiyo huku ikiwa tayari imemnasa Yusufu Kagoma kutoka Singida Fountain Gate Fc.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited