Home Makala Mzungu Yanga Atoa Tamko

Mzungu Yanga Atoa Tamko

by Sports Leo
0 comments

Mambo ni moto katika uongozi wa Yanga kwenye harakati za kutaka kubadilisha mfumo wa uendeshwaji kwenda kibiashara zaidi.

Uongozi huo ulimshusha juzi nchini Cerraca Antonio Pinto kutoka Ureno kwa ajili ya kuja kusimamia mchakato wa mabadiliko kwani amewahi kuwa mtendaji mkuu wa vigogo wa Ureno Benfica.

Pinto baada ya kutua nchini alimshukuru Mungu kwa kufika salama nchini na alichoweza kuwaambia Wanayanga ni kwamba wategemee kupata mambo mengi ambayo yataifanya klabu yao kuwa moja kati ya klabu kubwa Afrika.

banner

“Nitahakikisha nafanya kazi iliyonileta kwa umakini mkubwa na ni matumaini yangu kila kitu kitakuwa sawa na kuifanya iweze kujiendesha kibiashara katika soka la kimataifa,” alisema Pinto

Pinto anatarajiwa kukutana na uongozi wa klabu hiyo leo na kufanya kikao maalam kabla ya kuanza kuifanya kazi yake iliyomleta klabuni hapo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited