BAADA ya mchezo wao wa marudiano dhidi ya Al Rabita ya Sudan Kusini uliotarajiwa kuchezwa Desemba 6 kufutwa na Shirikisho la Soka Afrika,(Caf) timu hiyo imesonga mbele na inakutana na timu ya Sudan.
Namungo inayonolewa na Kocha Mkuu, Hemed Morroco mchezo wa awali ilishinda mabao 3-0 , Uwanja wa Azam Complex na mchezo wa marudio ulitarajiwa kuchezwa Azam Complex.
Taarifa rasmi iliyotolewa na Shirikisho la Soka Tanzania, (TFF) imesema kuwa Namungo imesonga mbele hatua ya pili ya mchujo Kombe la Shirikisho na itacheza na El Hilal Obeid ya Sudan.
Mchezo wa awali unatarajiwa kuchezwa Desemba 23 na ule wa marudio unatarajiwa kuchezwa Kati ya Sudan Januari 5 na 6.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
cc:Salehejembe