Home Makala Namungo Watoboa Caf Kukutana na Wasudan

Namungo Watoboa Caf Kukutana na Wasudan

by Dennis Msotwa
0 comments

BAADA ya mchezo wao wa marudiano dhidi ya Al Rabita ya Sudan Kusini uliotarajiwa kuchezwa Desemba 6 kufutwa na Shirikisho la Soka Afrika,(Caf) timu hiyo imesonga mbele na inakutana na timu ya Sudan.

Namungo inayonolewa na Kocha Mkuu, Hemed Morroco mchezo wa awali ilishinda mabao 3-0 , Uwanja wa Azam Complex na mchezo wa marudio ulitarajiwa kuchezwa Azam Complex.

Taarifa rasmi iliyotolewa na Shirikisho la Soka Tanzania, (TFF) imesema kuwa Namungo imesonga mbele hatua ya pili ya mchujo Kombe la Shirikisho na itacheza na El Hilal Obeid ya Sudan.

banner

Mchezo wa awali unatarajiwa kuchezwa Desemba 23  na ule wa marudio unatarajiwa kuchezwa Kati ya Sudan Januari 5 na 6.

cc:Salehejembe

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited