Home Makala Ni Azam Fc Tena,Yanyakua Tatu Rukwa

Ni Azam Fc Tena,Yanyakua Tatu Rukwa

by Sports Leo
0 comments

Azam Fc imeibuka leo na ushindi wa bao 1-0 mbele ya Tanzania Prisons kwenye mchezo wa ligi kuu bara uliochezwa uwanja wa Nelson Mandela, Rukwa.

Bao pekee la ushindi limepachikwa na Prince Dube dakika 90 kwa kichwa akiwa ndani ya 18 na kufanya kikosi chake kuibuka washindi kwa kujipatia bao la ugenini huku wakinyakua pointi tatu muhimu.

Azam FC inaweka rekodi ya kushinda mechi zake mbili mfululizo ikiwa ugenini baada ya kuanza kushinda mbele ya Mbeya City Uwanja wa Sokone kwa bao 1-0 na leo mbele ya Tanzania Prisons kwa bao 1-0.

banner

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited