Home Makala Ninja Ajifunga Yanga Miaka Miwili

Ninja Ajifunga Yanga Miaka Miwili

by Sports Leo
0 comments

Beki wa kati Abdallah Haji Shaibu ‘Ninja’ amesaini dili la miaka miwili leo Agosti 6 kuitumikia klabu ya Yanga akitokea MFK Vyskov ya Serbia.

Ninja alirejea nyumbani Tanzania baada ya kukosa nafasi ya kikosi cha kwanza ndani ya MFK Vyskov na alianza majaribio ndani ya Yanga chini ya Luc Eymael aliyekuwa Kocha Mkuu wa Yanga ambaye amefutwa kazi Julai 27.

Hatimaye leo beki huyo ametambulishwa rasmi kurejea kwenye timu yake ya zamani na huu unakuwa ni usajili wa tano kwa Yanga ambayo ipo kwenye mchakato wa kuboresha kikosi.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited