Kiungo mshambuliaji wa zamani wa klabu za Simba sc na Yanga sc Haruna Niyonzima amerejea katika klabu ya As Kigali kama mchezaji huru kwa mara ya tangu tangu alipofanya hivyo mwaka 2019 na 2022.
Kiungo huyo Fundi raia wa Rwanda alicheza nchini katika klabu ya Yanga sc kwa miaka takribani nane kisha akajiunga na Simba sc ambapo hakudumu sana akarejea nchini kwa lo katika klabu ya As Kigali kisha akarudi Yanga sc kwa mkataba mfupi na kurudi tena As Kigali mwaka 2022.
Hata hivyo baada ya muda staa huyo alipata ofa katika klabu ya Al Ta’awon ya nchini Libya ambapo alidumu kwa siku 52 pekee na kuamua kuachana na klabu hiyo kutokana na kutofuata matakwa ya kimkataba.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
As kigali itafaidika na ujio wa Niyonzima kutokana na uzoefu wake klabuni hapo ambapo sasa wanajiandaa na michezo ya nusu fainali ambapo sasa iko katika nafasi ya nne ikiwa na alama 23.