Home Makala Pluijm Yupo Tayari Kurejea Yanga

Pluijm Yupo Tayari Kurejea Yanga

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa zamani wa Yanga ambaye ni Mholanzi, Hans Pluijm amefungukia hatma yake ya kurejea na kukinoa kikosi hicho kwa mara ya tatu baada ya tetesi nyingi kuzagaa kuwa jina lake litajwe kwenye orodha ya makocha wanaowaniwa na Yanga ,hii ni baada ya aliyekuwa kocha wa timu hiyo Mbelgiji Luc Eymael kufutwa kazi.
Pluijm amesema kuwa bado viongozi wa Yanga hawajamfuata kwa ajili ya kufanya mazungumzo lakini yupo tayari kurejea kukinoa kikosi hicho kwani hana timu yoyote anayoifundisha kwa sasa na uzuri ni kuwa anawafahamu wachezaji baadhi wa Yanga na alishafanya nao kazi hivyo hatakuwa na kazi kubwa.

Jina jingine la kocha  linalotajwa kwenye orodha ya makocha wanaotarajiwa kujiunga na Yanga katika msimu ujao ni Ernie Brandts raia wa Uholanzi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited