Home Soka Rasmi Pamba Jiji Yaachana na Goran

Rasmi Pamba Jiji Yaachana na Goran

by Sports Leo
0 comments

Uongozi wa Klabu ya Pamba Jiji ya jijini Mwanza umefikia maamuzi ya kuachana na kocha wake mkuu Goran Kopunovic na msaidizi wake Henry Mkanwa kutokana na matokeo yasiyoridhisha katika ligi kuu ya Nbc msimu huu.

Goran tayari ameshapewa taarifa hiyo huku akisubiri baadhi ya taratibu za fidia ili kuondoka nchini huku sasa timu hiyo imekabidhiwa kwa kocha Salvatory Edward ambaye alikua msaidizi wa Goran kabla ya kumtimua na kumleta Henry Mkanwa.

Pamba jiji iliyopanda daraja la ligi kuu msimu huu mpaka sasa imecheza michezo saba ikipata sare nne na kufungwa michezo mitatu ikiwa mkiani mwa msimamo wa ligi kuu ya Nbc nchini.

banner

Pamoja na kuwa na uchumi unaoridhisha ikiwa chini ya Jiji la Mwanza klabu hiyo imekua haipati matokeo sahihi nyumbani na ugenini huku sababu kubwa ikitajwa ni mpasuko uliopo klabuni humo upande wa utawala kutokana na masuala ya udhamini.

Kwa mwenendo wa ligi ulivyo endapo klabu hiyo itashindwa kurejesha makali yake basi inaweza kushuka daraja kutokana na timu nyingi kuwa zimejipanga kupata matokeo msimu huu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited