Home Makala Ripoti ya Nabi Yanga sc Hadharani

Ripoti ya Nabi Yanga sc Hadharani

by Dennis Msotwa
0 comments

Kocha mkuu wa klabu ya Yanga Nasreddine Mohamed Nabi tayari ameshakabidhi ripoti kwa uongozi wa klabu kwa ajili ya msimu ujao katika ripoti hiyo kocha Nabi anahitaji kusajili wachezaji 8 wa nguvu ili kuendana na ushindani uliopo kwenye ligi kuu Tanzania Bara (VPL) na mechi za kimataifa msimu ujao.
Katika ripoti hiyo Nabi ameorodhesha wachezaji hao ni golikipa mmoja, mabeki watatu (wa kulia, kushoto na Kati) kiungo mchambuliaji mmoja, winga mmoja na washambuliaji wawili wa nguvu katika wachezaji hao Nabi anataka wachezaji 5 wawe wa kimataifa huku 3 wazawa.
Pia Kocha huyo amependekeza kuachwa kwa wachezaji wanne wa kimataifa na wachezaji watano wazawa Yanga tayari imeanza kusajili baada ya kumalizana na Beki wa kulia wa Djuma Shaban raia wa DRC Congo na Sasa inafanya mazungumzo na wachezaji wengine ili kukamilisha usajili uliotajwa na kocha.
Credit:Anderson

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited