Manchester United inadaiwa kumueka sokoni beki wake wake wa kati, Chris Smalling ambaye anahitajika na klabu As Roma,na Inter Milan.
Smalling aliwahi kuichezea Roma kwa mkopo msimu uliopita katika mechi 37 za mashindano yote,hivyo kwa sasa pia klabu hiyo ipo tayari kumsajili moja kwa moja kwa mkataba nyota huyo ingawa hawajafikia dau lililowekwa na Manchester United ambalo ni pauni 18 millioni.
Roma kwa sasa ina Pauni 13 millioni na haipo tayari kuongeza kiasi kingine kutokana na tayari wameshaongeza wachezaji wawili katika safu ya ulinzi ambao ni Hellas Verona na Marash Kumbulla.
Â