Home Makala Ronaldo Aikoa Man Utd

Ronaldo Aikoa Man Utd

by Sports Leo
0 comments

Cristiano Ronaldo amefanikiwa kuikoa klabu ya Man utd na kipigo baada ya kusawazisha bao dakika ya 62 na kuifanya Man united iambulie sare katika mchezo wa ligi kuu nchini Uingereza dhidi ya Chelsea uliofanyika katika uwanja wa Old Trafford jijini Manchester.

Marcos Alonso aliifungia Chelsea bao lililodumu kwa dakika mbili na kusawazishwa na Ronaldo dakika ya 62 akipokea pasi kutoka kwa kiungo Nemanja Matic huku wageni wakiukamata mchezo kwa kushambulia kwa kasi japo walikosa nafasi nyingi za wazi.

Usajili wa Ronaldo umeendelea kuwalipa Man United ambapo mpaka sasa amefunga mabao 17 huku katika mabao tisa ya klabu hiyo katika ligi kuu nchini Uingereza staa huyo amefunga mabao 8 peke yake na kumfanya kuwa mchezaji muhimu klabuni hapo.

banner

Man united sasa wanafikisha alama 55 katika michezo 35 wakiwa nafasi ya sita ya msimamo huku Chelsea wakiwa nafasi ya tatu na alama 66 katika michezo 33 ya ligi kuu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited