Home Makala Sababu Ya Kutokufika Kambini,Mkude

Sababu Ya Kutokufika Kambini,Mkude

by Sports Leo
0 comments

Jonas Mkude ambaye ni winga wa Simba  ameeleza sababu kubwa iliyomfanya ashindwe kujiunga na timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ ni matatizo ya kibinadamu yanayomkabili na siyo suala la utovu wa nidhamu.

Nyota huyo alichelewa kujiunga na timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars iliyokuwa imeweka kambi kwa ajili ya kujiwinda na michuano ya CHAN iliyotarajiwa kufanyika nchini Cameroon  kabla haijaahirishwa kutokana na maambukizi ya virusi vya Coronavilivyoingia duniani.

“Haina maana kwamba mimi ni mtovu wa nidhamu ndio maana nilichelewa kujiunga na timu ya Taifa hapana ninaithamini kazi yangu lakini masuala ya kibinadamu ndiyo ambayo yamekuwa yakinitatiza na kushindwa kuwahi kwenye kambi”alisema Mkude

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited