Home Makala Sakho Aitwa Senegal

Sakho Aitwa Senegal

by Sports Leo
0 comments

Nyota wa klabu ya Simba Sc  Pape Ousmane Sakho ameitwa kwenye kikosi cha wachezaji 24 cha timu ya Taifa ya Senegal kinachonolewa na kocha Mkuu Aliou Cisse kwaajili ya mechi mbili za kufuzu AFCON 2023 dhidi ya Msumbiji.

Staa huyo kinda anaungana na mastaa wa ulaya wanaounda safu ya ushambuliaji kuelekea kwenye mchezo huo ambao ni Sadio Mane (Bayern), Boulaye Dia (Salerntana), Habib Diallo (Strasbourg), Bamba Dieng (Lorient), Iliman Ndiaye (Sheffield Utd).

Hii ni mara ya kwanza kwa staa huyo kuitwa katika kikosi cha wakubwa hasa kuelekea kujiandaa na michuano mikubwa barani Afrika kwa ngazi za timu za Taifa.

banner

Licha ya kuwa na kiwango kizuri chenye kupanda na kushuka kwa nyakati flani flani staa huyo ni mwenye kipaji na maarifa mengi hasa anapokua na mpira mguuni huku uwezo wake wa kukokota na kukimbia kwenye nafasi ukiwa juu.

Sakho ambaye sasa anatumikia msimu wake wa pili kunako klabu hiyo pia ni mshindi wa goli bora katika michuano ya Caf mwaka jana.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited