Home Makala Sakho Auzwa Ufaransa

Sakho Auzwa Ufaransa

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imefanikiwa kumuuza staa wake Pape Osmane Sakho kwenda  klabu ya Quevilly Rouen Metropole (QRM) inayoshiriki ligi ya daraja la kwanza ya nchini Ufaransa.

Pape anaondoka Simba sc baada ya kukaa klabuni hapo kwa misimu miwili huku alikua amesaliwa na mkataba wa mwaka mmoja.

Katika dili hilo Simba sc imepata takribani dola laki sita huku pia kukiwa na mgawo kwa chama cha soka cha Senegal na klabu yake ya zamani ya Fc Teungueth FC ya nchini Senegal nayo ikipata mgawo katika dili hilo.

banner

Kuondoka kwa mchezaji huyo hakukua na namna zaidi ya furaha kwa viongozi wa Simba sc kwani wamepata hela za kutosha huku pia wakiwa tayari wamemsajili Luis Miqqueson kwa ajili ya kuziba nafasi hiyo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited