Timu ya Taifa ya Misri imefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 5-4 kwa penati dhidi ya Ivory Coast katika mchezo wa hatua ya mtoano kombe la mataifa ya Afrika nchini Cameroon.
mchezo huo ulimaliza dakika 120 bila bao ndipo ikafuata hatua ya changamoto ya mikwaju ya penati ili kupata mshindi wa kwenda hatua ya robo fainali kuungana na timu za Morroco,Senegal,Tunisia wenyeji Cameroon ambapo katika mikwaju 5 ya Ivory Coast walikosa mkwaju mmoja wa Eric Baily ambaye penati yake iliokolewa na kipa wa Misri.
Licha ya Wilfred Zaha kufunga mkwaju wa mwisho wa Ivory Coast lakini ufundi wa Mo salah uliwapeleka Misri hatua ya robo fainali baada ya kufunga mkwaju wa mwisho.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Sasa Misri inasubiri mshindi kati ya Mali na Equatorial Guinnea ili kujua nani ambaye itakabiliana nae katika hatua ya robo fainali.