Home Makala Salamba Atua Misri

Salamba Atua Misri

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa klabu ya Namungo Fc Adam Salamba amesajili na klabu ya Ghazl-El Mahala inayoshiriki ligi kuu nchini Misri kwa mkataba wa mwaka mmoja ambapo ataungana na Mtanzania Himid Mao kuhudumu katika klabu hiyo inayoshiriki ligi kuu nchini Misri ikiwa imeanzishwa mwaka 1936.

Klabu hiyo ni moja ya klabu kongwe nchini humo ikiwa inapatikana maeneo ya El Mahalla El Kubra na imemaliza ligi kuu msimu uliopita katika nafasi ya 15 ikiwa na alama 36 katika michezo 34 ya ligi kuu nchini humo.

Salamba mchezaji wa zamani wa klabu ya Namungo Fc,Simba sc na Js Soura ya nchini Algeria anajiunga na klabu hiyo akiwa kama mchezaji huru baada ya kukaa bila timu kwa miezi ya hivi karibuni na tayari klabu hiyo imeshamtambulisha kwa mashabiki.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited