Home Makala Semedo Atimkia Wolves

Semedo Atimkia Wolves

by Sports Leo
0 comments

Beki wa kulia ambaye pia ni raia wa Ureno,Nelson Semedo ametua Wolverhampton Wanderers kwa mkataba wa miaka mitatu akitokea Barcelona.

Kocha wa Wolves,Nuno Espirito Santo amefurahi kutua kwa beki huyo kwani amekuwa akimsaka beki wa kujaza nafasi ya Matt Donerty aliyetua Tottenham mwezi uliopita.

Semedo ametua Wolves kwa kima cha bilioni 5.2 ambapo anakuwa mwanasoka ghali kusajliwa na klabu hiyo  baada ya Silva aliyehudumiwa kwa Bilioni 4.9.

banner

Usajili wa Semedo unakuwa wa tatu kwa Wolves tangu dirisha kubwa la usajili kufunguliwa ambapo wawili ni Fabio Silva akitokea Fc Porto na Ki-Jana Hoever akitokea Liverpool.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited