Home Makala Serikali Waishauri Yanga Kuachana Na Morrison

Serikali Waishauri Yanga Kuachana Na Morrison

by Sports Leo
0 comments

Rais wa awamu ya nne wa serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete ameishauri Yanga kuachana na mvutano wa suala la mchezaji, Bernard Morrison kwani suala la kuibiana wachezaji kwa Simba Sc na Yanga Sc halikuanza hivi karibuni bali ni kawaida yao.

Kikwete ameyasema hayo jana kwenye kilele cha wiki ya mwananchi ampabo alialikwa kama mgeni rasmi kwenye tamasha hilo lililofanyika uwanja wa Mkapa.

“Kwa kuwa ninyi mmeibiwa Morrison najua nanyi mtajipanga wakati mwingine tena mtaiba mchezaji wao mzuri ni kawaida,Kinachotakiwa ni kuibua vipaji wenyewe ndani ili iwe rahisi kuwapata nyota ndani ya nchi ila masuala ya kupelekana FIFA ni kupoteza tu”alisema

banner

Benard Morrison alitambulishwa kuwa mchezaji wa Simba kwenye kilele cha Simba day Agosti 22 Uwanja wa Mkapa huku Agosti 30 kwenye kilele cha wiki ya mwanachi alitambulishwa kuwa mchezaji wa Yanga kwa kuwa shauri lake limepelekwa Mahakama ya Usuluhishi wa Kimichezo,(Cas).

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited