Home Makala Serikali,Michezo Na Corona

Serikali,Michezo Na Corona

by Sports Leo
0 comments

Waziri Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Kassim Majaliwa amesema kuwa wanasitisha masuala yote yanayohusu mikusanyiko ya watu isiyo ya lazima ikiwa ni kujikinga na ugonjwa wa Corona.

“Tumesitisha michezo yote inayokusanya makundi ya watu kama vile Ligi Kuu ya Tanzania, Ligi Daraja la Pili, Ligi Daraja la Kwanza, lakini pia michezo ya shule za msingi (Umitashumta), michezo ya shule za Sekondari (Umiseta) pamoja na ile ya mashirika ya umma kwa kipindi cha mwezi mmoja kuanzia leo”alisema Majaliwa

“Kwa hiyo Wizara ya Habari na Utamaduni na Michezo yenyewe itawaandikia mashirikisho yake yote ya michezo ili kuwaambia kwamba kwa kipindi cha mwezi mmoja hiki watatakiwa kusimamisha ratiba hizo katika michezo inayochezwa kipindi hiki ili kupambana na virusi vya Corona”

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited