Home Makala Shangwe la Bongo Lawakuna Us Monastr

Shangwe la Bongo Lawakuna Us Monastr

by Sports Leo
0 comments

Rais wa klab ya US Monastir ya nchini Tunisia Ahmed Belli atoa pongezi kwa Yanga SC na mashabiki wake baada ya jana kupokea ‘kichapo’ cha mabao 2-0 kutoka kwa vinara hao wa NBC Premier league Yanga sc kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho barani Afrika.

Rais huyo alizungumza hayo mapema leo baada ya timu yake kuingia makubaliano na Singida Big Stars kwa ajili ya kushirikiana masuala mbalimbali ya soka ambapo alionekana kushangazwa na mzuka na shangwe za mashabiki wa soka nchini walizoonyesha katika mchezo huo kiasi cha kupoteza kwa mabao 2-0.

Singida Big Stars na klabu hiyo zimeingia makubaliano ya ushirikiano katika masuala mbalimbali ya soka katika maeneo ya ufundi,miundombinu na maendeleo kwa ujumla wake.

banner

Singida Big Stars ina uhakika wa mwakani kushiriki michuano ya kimataifa baada ya kuwa na uwezekano mkubwa wa Tanzania kuingiza timu nne katika michuano ya kimataifa.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited