Home Makala Simba Queens Wakwaa Kisiki

Simba Queens Wakwaa Kisiki

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Wanawake ya Simba queens imeshindwa kufuzu hatua ya fainali ya kombe la wanawake barani Afrika baada ya kufungwa 1-0 na timu ya wanawake  Mamelod Sundowns ya nchini Afrika ya kusini.

Simba queens inayoshiriki michuano hiyo kwa mara ya kwanza iliwashangaza wengi kutokana na kuonyesha kiwango bora katika michezo ya awali na kufanikiwa kufuzu hatua ya nusu fainali ambapo imekwaa kisiki hicho.

Kipindi cha kwanza kilimalizika kwa klabu hizo kwenda mapumziko ikiwa 0-0 lakini mambo yalibadilika kipindi cha pili dakika ya 75 baada ya shuti la Joyce Rabale kushinda kipa wa Simba queen na kujaa wavuni ambapo bao hilo lilidumu mpaka mwisho wa mchezo huo.

banner

Wadada hao wa Mamelodi Sundowns  walipiga jumla ya pasi 458 passes katika mchezo huo ikilinganishwa na pasi 266 zilizopigwa na Simba Queens.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited