Home Makala Simba Sc Kileleni Nbc

Simba Sc Kileleni Nbc

by Dennis Msotwa
0 comments

Baada ya kufanikiwa kuchukua alama tatu katika mchezo wa pili wa ligi kuu dhidi ya Dodoma Jiji Fc klabu ya Simba sc sasa imefanikiwa kukaa kileleni mwa ligi kuu ya soka ya Nbc nchini.

Simba sc iliibuka na ushindi wa mabao mawili katika mchezo huo uliochezwa katika uwanja wa uhuru jijini Dar es salaam mabao yakifungwa na Jean Baleke dakika ya 43 na Moses Phiri dakika ya 55 na kupeleka furaha kwa mashabiki wa klabu hiyo ambao hawakujitokeza kwa wingi kama ilivyo kawaida yao.

Safu ya ulinzi ya Simba sc pamoja na kufanya vibaya dhidi ya Mtibwa Sugar na kuruhusu mabao mawili jana ilifanya vizuri ikiwa chini ya Che Malone Fondoh na Kennedy Juma huku pembeni wakicheza Shomari Kapombe na Mohamed Hussein na eneo la kiungo walitawala Mzamiru Yassin na Fabrice Ngoma.

banner

Sasa Simba sc kutokana na ushindi huo imefikisha alama sita kileleni mwa msimamo huku ikiwa jumla imefunga mabao sita katika ligi kuu na kufungwa mabao mawili.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited