Home Makala Simba sc Kukodi Pipa

Simba sc Kukodi Pipa

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imepanga kukodi ndege kuelekea nchini Angola katika mchezo wa ligi ya klabu bingwa barani Afrika dhidi ya klabu Premiero De Augosto wa raundi ya pili ya michuano ya hiyo mikubwa kwa ngazi za vilabu barani Afrika.

Simba sc imepanga kuingia nchini humo masaa machache kabla ya mchezo na baada ya mchezo kuwahi kurudi nyumbani mapema kujiandaa na mchezo wa marudiano hapa nchini baada ya wiki moja huku pia ikilazimika kutumia usafiri huo kupunguza hujuma zitakazotokana na kukaa muda mrefu nchini humo.

Simba sc imeingia katika hatua ya pili ya michuano hiyo ikifanikiwa kuitoa timu ya Nyassa Big Bullets ya nchini Malawa kwa jumla ya ushindi wa mabao 4-0 ikishinda mabao 2 kote ugenini na nyumbani.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited