Home Makala Simba sc Kuwavaa Wamalawi

Simba sc Kuwavaa Wamalawi

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imepangwa kuanza na Nyasa Big Bullets ya nchini Malawi katika mchezo wa hatua ya awali ya michuano ya klabu bingwa barani Afrika katika droo iliyopigwa nchini Misri.

Endapo Simba sc itafanikiwa kuitoa timu hiyo basi itakutana na mshindi kati ya Red Arrows ya nchini Zambia na Premiro Agosto ya nchini Angola.

Simba sc ina nafasi kubwa ya kuifunga Nyasa Big Bullets ambayo ipo juu ya kilele cha ligi kuu nchini humo ambayo inaendelea nchini Malawi huku pia ikiwa ni moja ya timu kongwe nchini humo ikianzishwa mwaka 1967 ambapo pia iliwahi kumilikiwa na rais wa zamani wa malawi Bakil Mluzi na kipindi hicho iliitwa Bakili Big Bullets.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited