Home Makala Simba sc Vs Al Ahly

Simba sc Vs Al Ahly

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Simba imepangwa kucheza na klabu ya Al-Ahly kwenye michuano ya African football league inayotarajiwa kufunguliwa hapa nchini siku ya 20 Oct 2023 katika uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar es salaam.
Mshindi katika mchezo huo  atakutana na mshindi baina ya Petro De Luanda  ya nchini Angola dhidi ya Mamelodi Sundowns ya Africa ya kusini a,bapo michuano hiyo inatarajiwa kuanzia hatua ya robo fainali huku ikishirikisha timu nane bora barani Afrika.

Simba sc inatarjiwa kupata upinzani mkali katika mchezo huo ikizingatiwa kiwango cha Al ahly katika michuano ya kimataifa huwa kiko juu huku wakiwana uzoefu wa kutosha kucheza hatua za mtoano hasa wakiwa wanaanzia ugenini na kumalizia nyumbani.

Ili ifuzu kwenda nusu fainali Simba sc haina budi kushinda mabao mengi hapa nyumbani kitu ambacho ni kigumu ikizingatiwa kuwa Al Ahly ina wachezaji wa viwango vya juu hasa Percy Tau ambaye alisajiliwa kutokea katika ligi kuu ya nchini Uingereza.

banner

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited