Home Makala Simba sc Vs Cska Moscow Dubai

Simba sc Vs Cska Moscow Dubai

by Dennis Msotwa
0 comments

Zikiwa zimesalia siku kadhaa kabla ya kurejea nchini klabu ya Simba sc imetangaza kuwa itacheza michezo miwili ya kirafiki ikiwa katika kambi ya maandalizi ya kumalizia awamu ya pili ya msimu wa ligi kuu pamoja na michuano ya kimataifa iliyoko Dubai nchi za falme za kiarabu.

Simba sc iliondoka nchini wiki iliyopita baada ya kutolewa katika michuano ya kombe la Mapinduzi ambapo kikosi hicho pamoja na kocha mpya Roberto Oliveira walipewa ofa hiyo ya kambi ili kocha huyo aweze kukaa na kikosi katika mazingira tulivu ili kuingiza mbinu zake kwa mastaa hao.

Simba sc kupitia mitandao yake ya kijamii imetangaza kucheza michezo miwili ya kirafiki katika kujaribu mbinu za kocha huyo ambapo timu hiyo itavaana na CSKA Moscow ya Urusi ambao ni mabingwa wa ligi ya klabu bingwa barani ulaya mwaka 2005 ambapo mchezo huo utafanyika Januari 15 huku mchezo mwingine dhidi ya timu ya Al Dhafra ukufanyika Januari 13.

banner

Baada ya michezo hiyo Simba sc itarejea haraka nchini kuja kuvaana na Mbeya city siku ya Jumanne januari 17 jijini Dar es salaam katika uwanja wa Benjamin Mkapa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited