Home Makala Simba sc Yaendeleza Dozi

Simba sc Yaendeleza Dozi

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Simba sc imeendeleza dozi ya mabao kwa timu ya Cosmopolitan Fc baada ya kuibamiza kwa mabao 5-1 katika mchezo wa kujipima nguvu ikijiandaa na michuano ya kimataifa hasa hatua ya pili ya michuano ya klabu bingwa barani Afrika na michuano mipya ya ligi inayojumuisha timu nane bora barani Afrika.

Juzi Simba sc iliibamiza Kipanga Fc kwa idadi ya mabao 3-0 yakifungwa na Moses Phiri,Aubin Kramo na Luis Miquissone na leo mapema imeibuka na ushindi huo kwa mabao ya Moses Phiri,Jean Baleke,Leandre Onana,Aubin Kramo na Shaban Idd Chilunda.

Simba sc itavaana na Power Dynamos ya Zambia katika mchezowa kuwania kufuzu hatua ya makundi ya klabu bingwa Septemba 17 nchini Zambia ambapo timu hizo zitarudiana nchini baada ya wiki mbili.

banner

Licha ya kuanza mdogomdogo kutafuta utimamu wa mwili baadhi ya mastaa wa Simba sc wameanza kuimarika hasa Luis Miqquisone ambaye usajili wake ulivuma sana hapa nchini kiasi cha wengi kumfuatilia zaidi.

“Jambo zuri ni baadhi ya wachezaji wetu kuanza kuimarika hasa Luis ambaye. ni mchezaji mkubwa na anajua kuamua mechi kama hizi sasa amepungua uzito anarudi kwenye kiwango chake huku pia Inonga amerejea na sasa tunasubiri kusikia kuhusu Aishi”Alisema kocha wa klabu hiyo Roberto Oliveira maarufu kama Robertinho wakati akiongea na mwandishi wetu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited