Klabu ya Simba sc imefanikiwa kuibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Malindi Fc katika mchezo wa kirafiki uliofanyika katika uwanja wa Amani mjini Unguja bao la Nassoro Kapama ambaye alifunga kwa kichwa kufuatia kona safi ya Pape Osmane Sakho dakika ya 13 ya mchezo na mpaka filimbi ya mwisho inapigwa matokeo yalibaki hivyo hivyo.
Simba sc iliyoanza na wachezaji wengi ambao hawapati nafasi mara kwa mara kikosini akiwemo golikipa Ally Salim,Dejan,Nassoro Kapama na Nelson Okwa pamoja na Peter Banda ambao walikua hawajachanganya na kusababisha mpira kuwa wa kawaida huku Malindi wakionyesha ushindani wa hali ya juu.
Mechi hiyo ni muendelezo wa maandalizi ya kujiandaa na raundi wa pili ya michuano ya kimataifa ambapo Simba sc itawavaa De Augosto kutoka Angola baada ya kufanikiwa kuwafunga Nyassa Big Bullets katika michezo yote miwili nyumbani na ugenini.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.