Home Makala Simba sc Yalamba Dili Nono

Simba sc Yalamba Dili Nono

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imefanikiwa kupata udhamini mnono wa kutoka kampuni ya kubashiri ya M-beti ambayo ndiyo itakua mdhamini mkuu wa klabu hiyo yenye jina kubwa Afrika kwa sasa.

Simba sc imepata udhamini wa miaka mitano kutoka kwa kampuni hiyo baada ya kumaliza mkataba na kampuni ya Sportspesa ambayo ilidhamini klabu hiyo pamoja na watani wao wa jadi Yanga sc kwa muda wa miaka mitano iliyopita kwa gharama ya shilingi bilioni 5 kwa kila mmoja.

Yanga sc yenyewe iliamua kuendelea na udhamini wa kampuni ya Sportspesa ambayo imeweka kiasi cha shilingi bilioni 12 kwa mkataba wa miaka mitatu huku Simba sc ambayo imeamua kuingia makubaliano na wapinzani wa kampuni hiyo ambayo ni M-bet wenyewe watalamba kiasi cha bilioni 26 katika mkataba wa miaka mitano.

banner

Kampuni hiyo inaingia kama mdhamini mkuu wa klabu hiyo baada ya kumaliza mkataba wake na Sportpesa na mgawanyo wa fedha utakuwa kama ifuatavyo;

Mwaka wa kwanza – Sh4.670 bilioni
Mwaka wa pili – Sh4.925 bilioni
Mwaka wa tatu – Sh5.205 bilioni
Mwaka wa nne – Sh5.514 bilion
Mwaka wa tano – Sh5.853 bilioni.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited