Home Makala Simba sc Yaleta Mbrazil kuwanoa Kina Manula

Simba sc Yaleta Mbrazil kuwanoa Kina Manula

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba imekamilisha usajili wa kocha wa makipa Milton Nienov raia wa Brazil kuchukua nafasi ya Mohamed Mwalami aliyefutwa kazi tangu October 29 mwaka Jana.

Milton ambaye amewahi kuzifundisha timu za Free State, Polikwane na Golden Arrows za Afrika kusini yupo jijini Dar Salaam muda wowote kuanzia sasa atatambulishwa kuwa kocha wa makipa wa klabu ya Simba kwa mkataba wa miaka miwili.

Kocha huyo atakua na jukumu kubwa la kuwanoa makipa Aishi Manula na Beno Kakolanya kuhakikisha wanapambana na mastraika wasumbufu katika hatua ya makundi ya klabu bingwa barani Afrika.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited