Home Makala Simba sc Yapaa Dubai

Simba sc Yapaa Dubai

by Sports Leo
0 comments

Mastaa wa klabu ya Simba sc jioni ya leo wamepaa kwa ndege ya shirika la Emirates kuelekea nchini Dubai kwa ajili ya kambi ya siku kumi kujiandaa ni michuano ya kimataifa pamoja na ligi kuu nchini.

Kikosi hiko kimepaa baada ya kutolewa katika michuano ya kombe la Mapinduzi ambapo lengo kuu la ziara hiyo ni kumpa nafasi kocha mpya Robertinho aliyejiunga na timu hizo wiki hii akitokea Vipers Fc kujuana kwa undani zaidi na wachezaji ili asipate shida katika kupanga kikosi katika mechi.

Mastaa wa kikosi hicho karibia wote wamesafiri kutokea hapa nchini huku wachache wakitarajia kuungana na kikosi kutokea makwao walipokua wameenda kwa mapumziko mafupi.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited