Home Makala Simba sc Yapata Ceo

Simba sc Yapata Ceo

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imemtangaza Iman Kajula kuwa bosi mpya wa klabu hiyo kwa kipindi cha miezi sita ijayo akichukua nafasi ya Barbara Gonzalez ambaye alijiuzuru nafasi hiyo hivi karibuni.

Kajuna ametangazwa leo kupitia vyanzo vya habari vya klabu hiyo ambapo atakua na jukumu la kusimamia uendeshaji na shughuli mbalimbali za klabu kama mtendaji mkuu wa klabu hiyo huku pia akihakikisha makombe yanarudi klabuni hapo kama ilivyokua hapo awali.

Kajuna ambaye kimsingi ni mwanachama na shabiki kindakindaki wa klabu hiyo anatajwa kuwa na uzoefu katika uongozi wa ngazi za juu akiwa bosi wa masoko na mawasiliano kwa nyakati mbalimbali katika benki za Crdb,Nmb na benki ya Posta huku pia kwa sasa akiwa ni mtendaji mkuu wa kampuni ya EAG Group.

banner

Simba sc sasa itakua imeongozwa kwa ujumla na Watendaji wakuu watatu akianza Senzo Mazingisa kisha Barbara na sasa ni Iman Kajula.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited