Home Makala Simba Sc Yapigwa Faini TPLB

Simba Sc Yapigwa Faini TPLB

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya soka ya Simba, imetozwa faini ya shilingi milioni moja (1,000,000) kwa kosa la walinzi wake kuwazuia walinzi wa uwanjani (stewards) kumkamata shabiki aliyekuwa akitaka kuingia kiwanjani baada ya mchezo wao dhidi ya Singida Black Stars uliopigwa Desemba 28, 2024.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) naye Kocha Robert Matano wa Fountain Gate FC, ametozwa faini ya shilingi laki tano (500,000) kwa kosa la kuwashutumu waamuzi waliochezesha mechi yao dhidi ya Simba SC iliyopigwa Februari 6, 2025.

Katika mchezo huo Simba sc ilipoteza alama moja baada ya kutoka sare ya 1-1 na Fountain Gate Fc kiasi cha kusababisha hali ya hewa kuchafuka katika mitandao ya kijamii.

banner

Pamoja na hilo sasa tayari klabu hiyo imerejea kileleni mwa msimamo baada ya kuinyika Tanzania Prisons kwa mabao 3-0 katika uwanja wa Kmc siku ya Jumatano.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited