Home Makala Simba sc Yasajili Kimya Kimya

Simba sc Yasajili Kimya Kimya

by Sports Leo
0 comments

Ni mwendo wa kimya kimya ndio ambao viongozi wa klabu ya Simba sc wameuchagua baada ya kufanya sajili takribani tano lakini mpaka sasa wahajazitangaza kokote Sportleo imebaini.

Tayari klabu hiyo kupitia kwa mwenyekiti wa bodi Salim Abdalah ”Try Again”imemalizana kwa kuwapa mikataba Moses Phiri ambaye tayari imemtambulisha kwa mashabiki wa klabu hiyo kama usajili wa kwanza huku pia ikiwa imewasainisha mikataba Habib Kyombo ambaye awali alisaini Singida Big Stars lakini Simba sc ikatumia ukubwa wake kubadili mawazo ya mchezaji na kumfanya akanunue mkataba wake kule Singida Big Stars.

Pia kiraka Nassoro Kapama nae tayari amesaini klabuni hapo akiwa kama mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake Kagera Sugar na tayari klabu yake ya zamani imeshamtakia kila la kheri katika malisho yake mapya huku Msimbazi japo klabu haijatangaza ikiwa imefanya kimya kimya kama ilivyo sera yao ya usajili ya sasa.

banner

Kwa upande ya sajili za kimataifa mbali na Phiri pia klabu hiyo imewasajili viungo washambuliaji Augustine Okrah na Nelson Okwa kutoka Afrika Magharibi pamoja na mshambuliaji wa Vipers Fc Cesar Manzoki ambaye alitua kimya kimya kusaini na kuondoka kimya kimya.

Sambamba na kusajili kimya kimya pia klabu hiyo imewaacha Meddie Kagere,Pascal Wawa,Yussuph Mhilu(Mkopo) huku pia panga likiendelea kwa mastaa wengine ili kuhakikisha usajili unakwenda sawa ili kushindana katika ngazi ya kimataifa ambapo awali waliishia robo fainali.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited