Home Makala Simba Warudisha Heshima

Simba Warudisha Heshima

by Sports Leo
0 comments

Katika michezo ya ligi kuu  bara inayoendelea Simba wamefanikiwa kurudisha heshima baada ya kuwafunga Mbao Fc mabao 2-1 katika uwanja wao wa nyumbani CCM Kirumba jijini Mwanza.

Hassan Dilunga anakuwa wa kwanza katika kipindi cha kwanza kuipatia Simba bao moja dakika ya 41 kwa kupeleka mashambulizi katika lango la Mbao kwa guu la kushoto lililomshinda  mlinda mlango wa Mbao.

Kipindi cha pili Jonas Mkude anaongeza bao la pili kwa Simba dakika ya 46 huku bao la kufutia machozi kwa Mbao walio chini ya Hemedi Moroco lilifungwa na Waziri Jr dakika ya 52.

banner

Simba Sc wanafikisha jumla ya pointi 38 ikiwa nafasi ya kwanza katika mechi ya 13 ikiwaacha wapinzani wake Yanga kwa pointi 13 na ikiwa na michezo miwili ili kuwa sawa na Simba.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited