Home Makala Singida Black Stars Yapoteza kwa Kmc

Singida Black Stars Yapoteza kwa Kmc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Singida Black Stars leo imekubali kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Kmc katika mchezo wa ligi kuu ya Nbc nchini uliofanyika katika uwanja wa Kmc Complex uliopo Mwenge jijini Dar es Salaam.

Kmc ikiwa nyumbani chini ya kocha Kally Ongara imebahatika kupata mabao hayo kipindi cha kwanza dakika za 35 na 40 yakifungwa na Oscar Paul aliyekua mwiba mchungu kwa Black Stars.

banner

 

Oscar alifunga bao la kwanza kutokana na kutumia vyema makosa ya mlinzi wa Singida Black Stars Anthony Bi Tra Bi aliyeshindwa kuokoa mpira uliokua unazagaa.

Bao la pili la lilitokana na pasi nzuri ya Daruweshi Saliboko aliyempasia vyema mfungaji na kumchambua golikipa wa Singida Black Stars Hussein Salum Masalanga.

Singida Black Stars hawakua na bahati baada ya Elvis Rupia kukosa penati dakika ya 48 ya mchezo kutokana na Augustine Sowah kuangushwa ndani ya eneo la hatari.

Mpaka dakika 90 zinakamilika wenyeji Kmc walifanikiwa kuchukua alama zote tatu na kufikisha alama 22 katika michezo 18 ya ligi kuu wakisimama katika nafasi ya sita ya msimamo.

Singida Black Stars wenyewe wameendelea kusalia katika nafasi ya nne wakiwa na alama 34 katika michezo 18 ya ligi kuu ya Nbc nchini.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited