Home Makala Suprise Kibao Singida Big Stars

Suprise Kibao Singida Big Stars

by Sports Leo
0 comments

Timu ya soka ya Singida Big Stars imefanya tamasha la kufungua msimu mpya la Singida Big day lililofanyika katika uwanja wa Liti mkoani humo ambapo mastaa kibao walitambulishwa.

Licha ya msanii Harmonize kutumbuiza katika tamasha hilo pia mashabiki wa soka mkoani humo walipata furaha zaidi kutokana na kufahamu kuwa kocha Hans Van De Pluijm kuwa ndie kocha mkuu wa klabu hiyo akisaidiwa na Nizar Khalfan na Mathias Lule huku pia Meddie Kagere na Paschal Wawa wakitambulishwa kuwa wachezaji wapya wa timu hiyo.

Suprise nyingine ni uwepo wa mastaa watatu kutoka nchini Brazil ambao nao wanaonekana wana viwango vizuri kiasi cha kucheza mpira mkubwa wakati wa mechi ya kirafiki dhidi ya Zanaco Fc iliyomalizika kwa wenyeji kushinda bao moja kwa bila likifungwa na Deus Kaseke.

banner

Singida Big Stars imepanda daraja kucheza ligi kuu msimu huu ambapo mpaka sasa imesajili mastaa waliotamba katika ligi kuu nchini akiwemo Amis Tambwe,Said Ndemla,Juma Abdul,Yassin Mustapha,Paulo Godfrey na wengineo wengi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited