Kocha mkuu wa Simba Sc Sven Vandenbroeck ametaja kuwa uchezaji wa haraka wa kutumia mfumo wa 4-3-3 ndiyo silaha inayomfanya ang’ae na kupata matokeo mazuri katika mechi anazoenda kupambana nazo.
Sven amebainisha kuwa katka mechi tano za ligi alizosimamia Simba ameweza kishinda mechi nne na kuusanya pointi 12 huku akiwa ametoka sare na Yanga pia kupoteza mchezo mmoja kwenye kombe la mapinduzi wakiwa wamefungwa bao 1-0 na Mtibwa Sugar.
“Mfumo wangu wa 4-3-3 ambao ndio ninaoutumia kila mechi,na mara zote nacheza kwa mfumo huo ndio unaotupatia ushindi hadi sasa”alisema Sven Vandenbroeck kutoka Ubelgiji.