Home Makala Tambwe Atemwa Singida Big stars.

Tambwe Atemwa Singida Big stars.

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Singida Big Stars iko mbioni kumalizana na mshambuliaji Amis Tambwe kwa lengo la kuvunja mkataba baada ya kutoridhishwa na kiwango cha mchezaji huyo aliyeisaidia timu hiyo katika kupanda daraja.

Tambwe mchezaji wa zamani wa Yanga sc amekosa nafasi mbele ya mastaa wenzie Meddie Kagere na Fancy Kazadi ambao kocha Hans Van de Pluijm amekua akiwatumia mara kwa mara kama washambuliaji wake kikosini humo.

“Tambwe pia hataweza kucheza msimu ujao, alitakiwa kuondoka tangu dirisha dogo lakini makubaliano hayakwenda vizuri kama tulivyokuwa tunatarajia.” kilisema chanzo hicho ambacho hakikutaka jina lake litajwe hadharani.

Pamoja na Tambwe pia walima alizeti hao wapo mbioni kuachana na mchezaji raia wa Brazil Dario Federico baada ya benchi la ufundi kuamua kuachana nae huku wakijiandaa kusajili beki mmoja na mshambuliaji mmoja kwa ajili ya michuano ya kimataifa.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited