Home Makala Tape Aondoka Azam Fc

Tape Aondoka Azam Fc

by Sports Leo
0 comments

Uongozi wa klab ya Azam na Mchezaji wao Tape Edinho wamefikia makubaliano ya pande zote mbili Juu ya kuvunja mkataba uliosalia wa mwaka mmoja wa staa huyo raia wa Ivory Coast.

Tape amelipwa Stahiki zake zote na  kupewa baraka za kwenda kutafuta changamoto sehemu nyingine baada ya kocha Yousuph Dabo kujiridhisha kuwa hana mpango nae baada ya kukaa nae siku kadhaa katika kambi ya klabu hiyo nchini Tunisia.

Pia kutemwa kwa mchezaji huyo kumechangiwa na kuzidisha idadi ya wachezaji wa kigeni ambao kwa mujibu wa kanuni wanapaswa kuwa 12 pekee ambapo klabu hiyo ilikua nao jumla 14.

banner

Tape alisajiliwa msimu uliopita pamoja na Kipre Jr ambapo baada ya nusu msimu alitolewa kwa mkopo kunako klabu yake ya zamani nchini Ivory Coast ya Stella Club d’Adjameambapo alikaa kwa kipindi cha miezi sita na kisha kurejea klabuni hapo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited