Mshambuliaji Tariq Seif huenda akapewa nafasi ya kuongoza safu ya ushambuliaji kwenye mchezo dhidi ya Mbeya City baada ya kupona majeraha
Jana Tariq alikuwa miongoni mwa wachezaji wa akiba hata hivyo hakupata nafasi ya kucheza.
Eymael alifafanua kuwa kutokana na mchezo ulivyokuwa ukiendelea, aliona haikuwa sahihi kumuingiza Tariq
“Nilipanga kama tungefunga mabao mawili angeingia. Najua mashabiki wana shauku kubwa ya kumuona tangu arejee kutoka majeruhi. Lakini atakuwepo kwenye mchezo ujao,” alisema kocha huyo raia wa Ubelgiji