Home Makala Tetesi Za Soka Ulaya

Tetesi Za Soka Ulaya

by Sports Leo
0 comments

Chelsea iko mbioni kumsajili kiungo wa Barcelona na Brazil ,Philippe Coutinho ambaye anacheza kikosi cha Baryen Munich kwa  mkopo.

Tottenham watamlenga beki wa kati Issa Diop na mshambuliaji wa Wolves na Mexico,Raul Jimenez katika uhamisho wa gharama ya pauni milioni 96.9.

Wakala wa Jorginho amesema kuwa wataingia kwenye mazungumzo kuhusu mkataba mpya na Chelsea baada ya kuwepo kwa tetesi kuwa Raul Jimenez atamfuata kocha wa zamani Maurizio Sarri huko Juventus.

banner

Mshambuliaji wa RB Leipzig raia wa Ujerumani ,Timo Werner anaweza kuwa anajiandaa kwa uhamisho kuelekea ligi kuu ya England kutokana na kuanza masomo ya lugha ya kiingereza ,huku Liverpool na Chelsea wakiwa wanamtaka mchezaji huyo.

Real Madrid wanajiandaa kumbakisha Gareth Bale kwenye msimu ujao pia wanajiandaa kutoa ofa ya mshambuliaji wa Serbia ,Luka Jovic kwenda Napoli likiwa ni jaribio la kushusha gharama ya pauni milioni 70 ya mchezaji wa miaka 24,Fabian Ruiz ambaye ananyemelewa na Manchester City.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited