Home Soka TPLB Yabariki Yanga Sc Kuhamia Kmc Stadium

TPLB Yabariki Yanga Sc Kuhamia Kmc Stadium

by Dennis Msotwa
0 comments

Bodi ya ligi kuu nchini (Tplb) imebariki uamuzi wa klabu ya Yanga sc kumtumia uwanja wa Kmc Complex uliopo Mwenge jijini Dar es Salaam kama uwanja wa nyumbani katika michezo yake iliyosalia ya ligi kuu ya Nbc nchini.

Awali klabu hiyo ilikua inautumia uwanja wa Azam Complex Chamazi jijini Dar es Salaam lakini baada ya kupoteza michezo miwili dhidi ya Klabu za Azam Fc na Tabora United moja kwa moja klabu hiyo itangaza kuhama uwanja na kuandika barua ya kuomba ridhaa kwa bodi hiyo yenye mamlaka ya kusimamia ligi kuu nchini.

banner

Taarifa kwa Umma iliyotolewa na bodi hiyo imeonyesha kukubali ombi la klabu hiyo kupitia kanuni ya 9:4 ya ligi kuu kuhusu uwanja.

Yanga sc baada ya kukubaliwa ombi hilo sasa itaungana na klabu za Simba sc,Kmc Fc,Simba queens na Yanga Princess kama timu zitakazo kuwa zinatumia uwanja huo kama uwanja wa nyumbani.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited