Mwenyekiti wa heshima wa klabu ya Simba sc na mfadhili wa klabu hiyo Mohamed Dewji amemchagua Salum Abdalah maarufu kama “Try Again” kuwa mwenyekiti wa klabu hiyo kwa mara ya pili baada ya muda wake kumalizika siku zilizopita.
Awali klabu hiyo ilifanya uchaguzi kuchagua viongozi wapya ambapo Murtaza Mangungu alishinda nafasi ya Mwenyekiti wa klabu hiyo kwa upande wa wanachama huku wajumbe kadhaa wakiongozwa na Asha Baraka wakichaguliwa katika uchaguzi huo uliokua na pilikapilika za kutosha.
Kwa upande wa Muwekezaji wa klabu hiyo Mohamed Dewji amemrejesha Try again kama Mwenyekiti wa klabu akimuwakilisha muwekezaji hiyo huku pia akiwafanyia tafrija fupi baadhi ya viongozi waliomaliza muda wao klabuni hapo hasa baada ya kuchaguliwa viongozi wapya.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.