Home Soka VAR Kutestiwa na Orlando

VAR Kutestiwa na Orlando

by Sports Leo
0 comments

Mitambo maalumu ya kumsaidia refa kutoa maamuzi sahihi katika michezo maarufu kama Var (Video Assistant Reffaree) tayari imeshafungwa katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam ambapo utafanyika mchezo kati ya Simba sc dhidi ya Orlando Pirates wa hatua ya robo fainali ya kwanza ya kombe la shirikisho.

Var inatarajiwa kufanyiwa majaribio leo saa moja usiku ambapo kutakua na mazoezi ya timu ya Orlando Pirates ambapo wamewasili usiku ya kuamkia leo wakitokea Nairobi Kenya.

Kwa mujibu wa taratibu za mitambo hiyo itafanyiwa majaribio kwa saa nne mfululizo kuona kama inafanya kazi kwa usahihi ili kuweza kuhimili kuchukua matukio yote ya mchezo huo siku husika.

banner

Hii ni mara ya kwanza kwa mitambo hiyo kutumika nchini tangu igunduliwe huku pia ikiwa ni mara ya kwanza kwa uwanja wa Benjamin Mkapa kufungwa mitambo hiyo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited