Home Makala Wachezaji Wawili Man Utd Watimuliwa Mazoezini

Wachezaji Wawili Man Utd Watimuliwa Mazoezini

by Sports Leo
0 comments

Wachezaji wa Manchester United ,Aaron Wan Bissaka na Timothy Fosu Mensah jumatatu ya wiki hii walitimuliwa na wafanyakazi wa shule St.Ambrose huko cheshire,Manchester baada ya kukutwa wakifanya mazoezi katika uwanja wa shule hiyo bila ruhusa.

Wachezaji hao walikuwa wakifanya mazoezi kwa kuzingatia sheria ya kupeana umbali lakini hata hivyo walijikuta wakiondolewa kwenye viwanja vya shule hiyo binafsi kwani hawakuwa na kibali maalum(ruhusa).

Ligi kuu ya England inatarajiwa kurejea mwezi Juni mosi licha ya wachezaji na viongozi kupinga mpango huo wa kurejea wakidai kuwa ligi irejee pale mambo yote yatakapokuwa shwari kwa kuisha kwa gonjwa la Corona kwani limekuwa tishio la dunia nzima.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited