Home Makala WaziriJr Atua Mbao Fc

WaziriJr Atua Mbao Fc

by Dennis Msotwa
0 comments

Mshambuliaji wa zamani wa Toto Africans ya Mwanza na Azam Fc Waziri Junior amejiunga na timu ya Mbao fc ya jijini Mwanza kwa mkataba wa mwaka mmoja.

Waziri aliibukia Toto Afrika ya Mwanza na kisha alisajililiwa na Azam fc japo hakupata nafasi ya kucheza kutokana na kukabiliwa na majeraha ya mara kwa mara mpaka alipotolewa kwa mkopo na matajiri hao wa chamazi.

Waziri mwenye uwezo wa kucheza kwa ufasaha nafasi za ushambuliaji wa kati atajiunga na timu hiyo mara baada ya kumalizika kwa kliniki ya michezo ya timu hiyo ya kutafuta vipaji inayofanyika katika uwanja wa Ccm Kirumba.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited