Home Makala Yanga Kibabe Wanyakua Wawili Congo

Yanga Kibabe Wanyakua Wawili Congo

by Sports Leo
0 comments

Yanga Sc imekamilisha usajili wa wachezaji wawili kwa mpigo kutokea nchini DR Congo kwenye klabu ya As Vita ambao ni Mukoko Tunombe na Tuisila Kisinda.

Wote wawili wamekubali kumwaga wino wa kuitumikia klabu hiyo kwa miaka miwili jana usiku na kutinga rasmi uzi wa Jangwani kuashiria ni miongoni mwao tayari kwa msimu wa 2020/2021.

Mkurugenzi wa uwekezaji wa GSM,Hersi Said ambaye pia anahusika zaidi kusimamia usajili wa wachezaji Yanga Sc ametumia takribani siku mbili kuwachukua wachezaji hao lakini bado kuna kifaa kingine wanakihitaji kutoka As Vita ambaye atahusika zaidi kufunga mabao.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited