Home Makala Yanga sc Haishikiki

Yanga sc Haishikiki

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc imezidi kuonyesha ubabe dhidi ya timu nyingine za ligi kuu baada ya kuifunga klabu ya Ruvu Shooting kwa mabao 2-0 katika mchezo hatari wa ligi kuu uliofganyika katika uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar es salaam.

Katika mchezo huo Yanga sc ililazimika kusubiri mpaka kipindi cha pili ili kupata bao la uongozi kupitia kwa Feisal Salum dakika ya 52 akifunga kwa kichwa krosi safi ya Joyce Lomalisa Mtambala kutokea upande wa kushoto wa uwanja bao ambalo lilirudisha morali kwa mashabiki wa klabu ya Yanga sc hali iliyopelekea kushangilia kwa nguvu na hatimaye kufanikiwa kupata bao la pili dakika ya 71 ya mchezo kupitia kwa Bakari Mwamnyeto.

Yanga sc kutokana na ushindi huo sasa imefikisha alama 13 ikiwa juu kileleni mwa msimamo wa ligi kuu nchini ikitanguliwa na Simba sc kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa huku wiki hii ikiwa na mchezo mgumu wa kimataifa dhidi ya Al Hilal siku ya jumamosi.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited